Monday, May 25, 2015

VAN DE VAART AICHOMOLEA AJAX.

WAKALA wa Rafael van de Vaart amebainisha kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Uholanzi hatarejea katika klabu ya Ajax Amsterdam kiangazi hiki. Mkataba wa sasa wa Van de Vaart katika klabu ya Hamburg unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa Juni mwaka huu na amekuwa akihusishwa na tetesi za kurejea Ajax ambako ndipo alipokulia na kuja kuwa kiungo bora kabisa Ulaya. Hata hivyo, wakala wa kiungo huyo, Roberto Geerlings amebainisha kuwa mteja wake hajaamua mahali anapotaka kwenda mpaka sasa. Wakala huyo amesema ni vyema kuihabalisha Ajax ili waweze kutafuta mbadala mwingine kwani kwa kipindi kirefu wamekuwa wakisubiri uamuzi wake.

No comments:

Post a Comment