Tuesday, April 19, 2016

TETESI ZA USAJILI ZILIZOJIRI HUKO MAJUU.

Maskauti wa Barcelona walikwenda nchini Ujerumani kumtizama Pierre-Emerick Aubameyang lakini walirejea wakiwa na malengo tofauti ya kumsajili beki wa kati Mats Hummels ambaye mkataba wake na Borussia Dortmund unatarajiwa kumalizika mwaka 2017.
Chanzo: Bild

KLABU ya Ajax Amsterdam inatarajiwa kumuwania Klaas-Jan Hunterlaar ambaye atamaliza mkataba wake na Schalke mwaka 2017. Mshambuliaji huyo ambaye anaweza kwenda kuziba nafasi ya Arek Milik anafahamu kuwa anawindwa na klabu hiyo.
Chanzo: Algemeen Dagblad

KLABU ya Real Madrid huenda ikamruhusu Lucas Silva kurejea nchini kwao Brazil katika klabu ya Cruzeira pindi mkopo wake katika klabu ya Marseille utakapomalizika.
Chanzo: L’Equipe

BEKI wa Corinthians, Fagner anatizamwa kwa karibu na klabu ya Barcelona ingawa hakuna mazungumzo yeyote yaliyofanyika na mchezaji huyo ambaye anatajwa kuwa atakuja kuziba nafasi ya dani Alves.
Chanzo: SporTV

KLABU ya Manchester City inadaiwa kumfukuzia chipukizi wa Celtic, Kieran Tierney baada ya beki huyo kuonyesha kiwnago bora katika mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Scotland dhidi ya Rangers. Liverpool na Southampton nazo pia zinatajwa kumuwania.
Chanzo: Daily Mail

No comments:

Post a Comment