Tuesday, August 30, 2016

ARSENAL KUMTOA WILSHERE KWA MKOPO.

KLABU ya Arsenal inadaiwa kuwa tayari kumuacha kiungo wa kimataifa wa Uingereza Jack Wilshere kuondoka kwa mkopo ili kupata nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24, ambaye amekuwa akisumbuliwa na majeruhi ya mara kwa mara, alifanikiw akucheza mechi tatu pekee kwa Arsenal msimu uliopita baada ya kuvunjika mfupa wa fibula. Wilshere ameichezea Uingereza mechi tatu kipindi cha kiangazi ikiwemo michezo mitatu ya michuano ya Ulaya lakini hajajumuishwa katika kikosi cha Sam Allardyce alichokitaja wiki hii. Kiangazi hiki Arsenal wamemsajili kiungo wa kimataifa wa Uswisi Granit Xhaka kwa kitita cha paundi milioni 35. Wilshere amebaki na saa 48 za kutafuta klabu ya kwenda kwa mkopo kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili la kiangazi.

No comments:

Post a Comment