KLABU ya Wolfsburg imefanikiwa kumsajili Jakub Blaszczykowiski kutoka Borussia Dortmund kwa mkataba wa miaka mitatu. Nyota huyo wa kimataifa wa Poland ambaye alijiunga na Dortmund mwaka 2007, amekamilisha mkataba wake huo wa moja kwa moja Wolfsburg ambao unakadiriwa kufikia euro milioni tano. Jakub mwenye umri wa miaka 30 anajiunga na klabu hiyo kuziba nafasi ya Andre Schurrle aliyekwenda Dortmund mapema kiangazi hiki. Mkurugenzi wa michezo wa Wolfsburg Klaus Allofs alithibitisha taarifa hizo na kuongeza kuwa winga huyo atasaidia sana klabu hiyo msimu ujao kutokana na ubora wake.
No comments:
Post a Comment