Monday, September 19, 2016

KLOPP ATAMBIA VIKOSI VYAKE.

MENEJA wa Liverpool, Jurgen Klopp amedai hana mpango wowote wa kuwapumzisha wachezaji wanaoonekana kuwa fiti wakati wa mchezo wao wa mzunguko wa tatu wa Kombe la Ligi dhidi ya Derby County. Klopp anaamini kuwa kila kikosi atakachokitumia msimu huu kitakuwa kiko vizuri. Liverpool wanatarajiwa kusafiri kwenda Pride Road kesho jioni kwa ajili ya mchezo huo ambapo watakuwa wakijaribu kuendelea rekodi yao nzuri ya kushinda mechi nne mfululizo zilizopita. Akihojiwa Klopp amesema kwa mawazo yake vikosi vyote alivyonavyo ni imara hivyo hana shaka na mchezo wao huo wa kesho.

No comments:

Post a Comment