Friday, April 21, 2017

JESUS AREJEA KUIPA NGUVU MAN CITY.

MSHAMBULIAJI wa Manchester City, Gabriel Jesus anaweza kuanza katika mchezo wa nusu fainali ya michuano ya Kombe la FA dhidi ya Arsenal Jumapili hii. Jesus amekuwa nje ya uwanja toka alipovunjika mfupa wa mguu katika mchezo wa dhidi ya Bournemouth Februari 13 mwaka huu. Nyota huyo wa kimataifa wa Brazil alitua kwa kishindo City na kupewa nafasi ya kuanza badala ya Sergio Aguero na kufanikiw akufunga mabao matatu kwenye mechi nne alizocheza. Mapema wiki hii Jesus alirejea mazoezini na meneja Pep Guardiola amesema anaweza kumjumuisha katika kikosi chake kwa ajili ya mchezo wao huo wa Jumapili katika Uwanja wa Wembley.

No comments:

Post a Comment