
Saturday, September 3, 2011
EURO QALIFIERS: UHOILANZI YAISHINDILIA SAN MARINO MABAO 11-0.
MATOKEO MENGINE YA MICHEZO EURO QALIFIER NI KAMA IFUATAVYO:
Israel 0 - 1 Greece
Lithuania 0 - 0 Liechtenstein
Finland 4 - 1 Moldova
Andorra 0 - 3 Armenia
Azerbaijan 1 - 1 Belgium
Russia 1 - 0 Macedonia
Georgia 0 - 1 Latvia
Malta 1 - 3 Croatia
Turkey 2 - 1 Kazakhstan
Belarus 0 - 2 Bosnia-Herzegovina
Luxembourg 0 - 2 Romania
Hungary 2 - 1 Sweden
Norway 1 - 0 Iceland
Bulgaria 0 - 3 England
Cyprus 0 - 4 Portugal
Faroe Islands 0 - 1 Italy
Germany 6 - 2 Austria Northern Ireland 0 - 1 Serbia
Republic of Ireland 0 - 0 Slovakia
Slovenia 1 - 2 Estonia
Wales 2 - 1 Montenegro
Albania 1 - 2 France
Wednesday, August 31, 2011
Tuesday, August 30, 2011
TAARIFA MBALIMBALI KUTOKA TFF.
VIINGILIO VYA STARS NA ALGERIA
Viingilio kwa ajili ya mechi ya mchujo kutafuta tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Equatorial Guinea na Gabon kati ya Taifa Stars na Algeria vitakuwa kama ifuatavyo;
Viti vya kijani ni sh. 3,000, viti vya bluu sh. 5,000, viti vya rangi ya chungwa sh. 7,000, VIP C sh.10,000, VIP B sh. 20,000 na VIP A sh. 30,000. Tiketi zitaanza kuuzwa Septemba Mosi mwaka huu.
Taifa Stars tayari iko kambini tangu jana (Agosti 28 mwaka huu) na inaendelea na mazoezi Uwanja wa Karume ambapo wachezaji wote wa ndani waliripoti jana mchana na kuanza mazoezi jioni.
Wachezaji wan je waliofika jana usiku ni Abdi Kassim na Dan Mrwanda kutoka Vietnam na Mbwana Samata kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. Athuman Machupa (Sweden), Henry Joseph (Norway) na Idrisa Rajab (Kenya) wanaingia leo jioni.
Nizar Khalfan wa Vancouver Whitecaps ya Canada ndiye atakayekuwa mchezaji wa mwisho kuripoti kambini. Khalfan atatua nchini kesho saa 5.15 usiku kwa ndege ya PrescisionAir akitokea Nairobi.
TWIGA STARS KUAGWA LEO
Timu ya Taifa ya wanawake ya mpira wa miguu (Twigs Stars) inayoondoka Agosti 31 mwaka huu kwenda Maputo, Msumbiji kwenye michezo ya All Africa Games itakayofanyika nchini humo kuanzia Septemba 3-18 mwaka huu itaagwa kesho (Agosti 30 mwaka huu).
Twiga Stars wataagwa saa 6 mchana kambini kwao hoteli ya Itumbi iliyopo Magomeni Mwembechai, Dar es Salaam. Wakati huo huo Kocha Mkuu wa timu hiyo Charles Boniface Mkwasa leo ametangaza majina ya wachezaji 16 watakaokwenda Maputo.
Wachezaji hao ni Sophia Mwasikili, Fatuma Omary, Mwanaidi Tamba, Fatuma Bashiri, Mwajuma Abdallah, Asha Rashid, Mwanahamisi Omari, Pulkeria Charaji, Ester Chabruma, Zena Khamis, Fridian John, Fatuma Mustafa, Ettoe Mlenzi, Ftuma Khatib, Maimuna Said na Mwapewa Mtumwa.
Viongozi watakaofuatana na timu hiyo ni Mkwasa, kocha msaidizi Nasra Mohamed, daktari wa timu Dk. Gania Seif wakati Meneja wa timu hiyo ni Furaha Francis.
Mechi ya kwanza ya Twiga Stars itakuwa Septembe 5 mwaka huu dhidi ya Ghana wakati ya pili dhidi ya Afrika Kusini itachezwa Septemba 8 mwaka huu. Twiga Stars itacheza mechi yake ya mwisho katika hatua ya makundi Septemba 11 mwaka huu dhidi ya Zimbabwe.
KOCHA WA UNDER 20 AITA 30.
DAR ES SALAAM, Tanzania
KOCHA wa timu za vijana Kim Poulsen ametangaza kikosi cha wachezaji 30 wa timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) kwa ajili ya mazoezi mwezi ujao.
Wachezaji walioitwa ni Saleh Ally (TSA), Jackson Wandwi (Azam), Hassan Kessy (Mtibwa Sugar), Khamis Mroki (Mtibwa Sugar), Yassin Mustapha (Polisi Dodoma), Andrew Kasembe (Moro United), Issa Rashid (Mtibwa Sugar), Ally Teru (Simba), Said Ruhava (Kagera Sugar), Samuel Mkomola (Azam), Frank Damayo (JKT Ruvu), Omega Seme (Yanga), Atupele Green (Yanga), Thomas Ulimwengu (ABC Sweden) na Jerome Lambele (Moro United).
Wengine ni Simon Msuvan (Azam), Ramadhan Singano (Simba), Alex Joseph (Majimaji), Ibrahim Rajab (Azam), Renatus Patrick (Polisi Dodoma), Abdallah Kilala (AFC), Rajab Zahir (Moro United), Amani Kyata (TSA), Edward Shija (Simba), Alfred Amede (Russia), Khelf Hassan (Kenya), Emily Mgeta (TSC Mwanza), Ramadhan Salum (Simba), Frank Sekule (Simba) na Hassan Dilunga (Ruvu Shooting).
Monday, August 29, 2011
FORLAN ATIMKIA INTER.
MILAN, Italia
Diego Forlan amethibitisha kuwa atajiunga na Inter Milan baada ya muda wake wa kubaki Atletico Madrid kuisha.
Uruguay straiker mwenye umri wa miaka 32 amefanya mkutano na waandishi wa habari na kueleza kwamba hatoendelea kuwepo ndani ya Uwanja wa Vincente Calderon kama mchezaji wa Atletico na sasa anaelekea jijini Milan kuitumikia klabu inayotumia uwanja wa Giuseppe De Maeaza.
Forlan sasa atasafiri kueleka Milan ambapo atafanyiwa vipimo vya afya na baadae kusaini mkataba wa kuitumikia Inter Milan.
“Naenda kujiunga na klabu kubwa na kuna changamoto kubwa mbele yangu.Nataka kumshukuru Massimo Moratti kwa nafasi hii.
“Nimeshaongea na Estaban Cambiasso na Diego Milito, wote ni marafiki zangu.Naifahamu Serie A kwa kuwa nimeshaangalia mechi nyingi kwenye TV na nina furaha kubwa kucheza nchini Italia baada ya Premier League na La Liga.” – Forlan
Subscribe to:
Posts (Atom)