Monday, October 31, 2011

POULSEN AITA 22 STARS.

Jan Poulsen
Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars JAN POULSEN ametangaza kikosi cha wachezaji 22 kwa ajili ya mchezo wa mchujo wa Kombe la Dunia dhidi ya Chad utakaochezwa Novemba 11 mwaka huu jijini N’Djamena.Katika kikosi hicho POULSEN amewaita kwa mara ya kwanza Golikipa MWADINI ALLY wa Azam na kiungo SHOMARY KAPOMBE kutoka Simba. Kikosi kamili cha timu hiyo kwa upande wa makipa ni JUMA KASEJA na MWADINI ALLY Walinzi ni AGGREY MORRIS, JUMA NYOSO , IDRISSA RAJAB, ERASTO NYONI, NADIR HAROUB, GODFREY TAITA na JUMA JABU.
Mwadini Ally
Kwa upande wa viungo yupo HENRY JOSEPH ,NURDIN BAKARI ,SHABANI NDITI ,ABDI KASSIM ,RAMADHAN CHOMBO na SHOMARI KAPOMBE . Washambuliaji ni NIZAR KHALFAN, MRISHO NGASSA, MBWANA SAMATA , DAN MRWANDA, ATHUMAN MACHUPA, HUSSEIN JAVU pamoja na THOMAS ULIMWENGU. Timu hiyo itaingia kambini Novemba 3 Jijini Dar es Salaam huku ikitarajia kuondoka nchini Novemba 9 mwaka huu ikiwa na msafara wa watu 35 kwenda N’Djamena kwa ajili ya mchezo huo. Timu hizo zitarudiana Novemba 15 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment