Monday, October 31, 2011

ZIMBABWE KUANDAA AFRICA WOMEN CHAMPIONSHIP.

SHIRIKISHO la Soka la Zimbabwe-ZIFA- limekubali kuwa mwenyeji wa michuano ya Afrika ya wanawake itakayofanyika 2012.Shirikisho hilo hivi sasa linasubiria jibu kutoka serikalini kabla ya mwezi Novemba kwa ajili ya kuandaa michuano hiyo.Zimbabwe wamepewa nafasi hiyo na Shirikisho la Soka la Afrika- CAF- baada ya kuandaa kwa mafanikio michuano ya wanawake ya Cosafa iliyofanyika mwezi Julai mwaka huu.Ofisa Mkuu wa ZIFA amesema michuano hiyo itasaidia kupandisha kiwango cha soka cha nchi hiyo pamoja na kufungua milango kwa watalii kumiminika kuitembelea nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment