Tuesday, November 22, 2011

BALLACK KUTIMIZA MECHI WA 100 KATIKA MICHUANO YA ULAYA.

NAHODHA wa Bayer Leverkusen Michael Ballack anatarajia kutimiza mechi yake ya 100 katika mashindano ya vilabu Ulaya wakati timu ya hiyo itapopambana na klabu yake ya zamani ya Chelsea katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya Jumatano hii. Chelsea inaongoza kwa alama 2 zaidi ya Leverrkusen katika kundi E na Ballack anategemea mchezo mgumu watakapokutana haswa baada ya timu hiyo kufungwa na Liverpool katika mchezo wa ligi. Kiungo huyo amesema Chelsea wanajua umuhimu wa mchezo leo hivyo kufanya timu hiyo kuwa hatari siku ya leo lakini wanaweza kuwafunga kwakuwa wanacheza wakiwa nyumbani na kila mtu anusubiria mchezo huo. Ballack alijiunga na Leverkusen mwaka 2010 kwa mara ya pili baada ya kuitumikia Chelsea kwa miaka minne na hivi sasa amerudi katika kiwango chake.

No comments:

Post a Comment