Thursday, November 24, 2011

KENYA KUANDAA CHALLENGE 2012.

Kenya inatarajiwa kuandaa michuano ya Kombe la Challenge ya Baraza la Vyama vya Michezo la nchi za Afrika Mashariki na Kati-CECAFA itakayofanyika mwaka 2012. Hatua ya kuiteua Kenya kuandaa michuano hiyo mwakani ilifikiwa Alhamisi hii katika mkutano wa uchaguzi wa baraza hilo uliofanyika Dar es Salaam. Rais wa Shirikisho la Soka la Kenya Sam Nyamweya alielezea kuteuliwa huko kuandaa michuano hiyo kama habari njema na kulishukuru baraza hilo kwa kuwaamini kuwa wenyeji. Nyamweya amesema kazi kubwa inabidi ianze sasa kwakuwa wanataka mji wa Kisumu uwe mmoja wapo utakaokuwa wenyeji wa michuano hiyo na mapema watakaporudi wataitaarifu manispaa ya mji huo kuanza maandalizi.



No comments:

Post a Comment