Monday, November 28, 2011

RAMBIRAMBI AZIDI KUMIMINIKA KUFUATIA KIFO CHA SPEED.

SALAMU za rambirambi zimeendelea kuminika kufuatia kifo cha aliyekuwa meneja wa timu ya Taifa ya Wales ambaye alikutwa amekufa akiwa nyumbani kwake. Kiungo huyo wa zamani mwenye miaka 42 ameichezea Wales michezo 85 na amekuwa akikinoa kikosi cha nchi hiyo katika michezo 10. Mojawapo ya watu walioguswa na kifo cha Speed ni pamoja na aliyekuwa meneja wa timu hiyo Mark Hughes, nahodha wa kikosi hicho Bobby Gould, Michael Owen, Waziri wa Michezo wan chi hiyo pamoja na rafiki wa karibu wa meneja huyo Graig Bellamy. Polisi walithibitisha kuwa mwili uligundulika nyumbani kwake katika mji wa Huntington ambapo alikutwa amejinyonga huku poilisi wakisema hakuna mtu yoyote anayehisiwa kufanya tukio hilo. Chama cha Soka cha nchi hiyo kimeelezea kusikitishwa na kifo cha mchezaji huyo ambapo katika taarifa yake kimesema huenda mchezaji mashuhuri wa zamani alijiua mwenyewe.

No comments:

Post a Comment