Tuesday, November 15, 2011

REAL-BARCA CLASICO DATE ANNOUNCED.

MCHEZO wa mahasimu wa soka nchini Hispania kati ya Real Madrid na Barcelona unatarajiwa kuchezwa Jumamosi Desemba 10 mwaka huu tarehe ambayo ilitangazwa jana. Madrid walikuwa wanataka mchezo huo uchezwe Jumapili mchana Desemba 11 ili wadau wao katika bara la Asia wapate kushuhudia mchezo huo. Hatahivyo Barcelona walipinga suala hilo na kusisitza mchezo huo uchezwe Jumamosi ili kutoa nafasi ya timu hiyo kuondoka mapema kwenda kujiandaa na michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia itakayofanyika Japan ambapo timu inatarajiwa kusafikiri asubuhi ya Jumapili mara baada ya mchezo huo wa jumamosi. Barcelona haijawahi kupoteza mchezo wowote wa Ligi Kuu ya Hispania-La Liga toka kocha wake Pep Guadiola alipochukua mikoba ya kuinoa klabu hiyo mwaka 2008 ingawa Madrid walifanikiwa kuifunga Barcelona katika mchezo mmoja wa Kombe la Mfalme. Madrid ndio wanaoongoza ligi kwasasa wakiwa na tofauti ya pointi 3 mbele ya mahasimu wao hao huku wakiwa wamebakisha michezo mitatu kabla hajakutana.

No comments:

Post a Comment