Friday, November 18, 2011

TENGA KUFUNGA KOZI YA CAF.

Rais wa TFF, Leodegar Tenga kesho atafunga kozi ya ukocha kwa ajili ya kupata leseni za daraja C kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) iliyofanyika kuanzia Novemba 7 mwaka huu. Ufungaji wa kozi hiyo iliyoshirikisha makocha 30 utafanyika kuanzia saa 4.30 asubuhi katika ofisi za TFF. Kozi hiyo iliendeshwa na wakufunzi wanne, mmoja wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), wawili wa CAF na mmoja wa Chama cha Mpira wa Miguu Denmark (DBU). Mkufunzi wa FIFA alikuwa Jan Poulsen, kutoka CAF ni Sunday Kayuni (Tanzania), Kasimawo Laloko (Nigeria) wakati kutoka Denmark ni Kim Poulsen. Makocha walioshiriki ni Christopher Eliakim, Jumanne Ntambi, Keneth Mkapa, Mussa Furutuni, Mecky Maxime, Gideon Kolongo, Maka Mwalwisi, Haji Amir, Tiba Mlesa, Stephen Matata, Wane Mkisi, Leonard Jima na Ahmed Mumba. Wengine ni Peter Mhina, Absolom Mwakyonde, Maarufu Yassin, Mussa Kamtande, Wilfred Kidau, Eliasa Thabit, Dismas Haonga, Fulgence Novatus, Juma Mgunda, Hassan Banyai, Mohamed Tajdin, Sebastian Nkoma, Emmanuel Massawe, Gabriel Gunda, Abdul Nyumba na Richard Kabudi.

No comments:

Post a Comment