Friday, November 18, 2011

WENGER AFURAHIA HENRY KUFANYA MAZOEZI NA VIJANA WAKE.

MENEJA wa timu Arsenal Arsene Wenger ana matumaini kuwa kuwepo kwa mshambuliaji wa timu hiyo wa zamani Thierry Henry katika mazoezi kutaongeza chachu ya ushindi katika kikosi chake ambacho kitapambana na Norwich kesho katika mchezo wa ligi. Henry mwenye umri wa miaka 34 ambaye pia aliwahi kuwa kuwa nahodha wa kikosi hicho amejiunga na klabu hiyo kwa ajili ya mazoezi ya kujiweka fiti wakati huu ambao timu yake ya New York Red Bulls imetolewa katika hatua ya mtoano wa ligi ya Marekani. Mshambuliaji huyo wa kimataifa kutoka Ufaransa aliondoka Arsenal na kuhamia Barcelona mwaka 2007 na Wenger alifurahi kumuona mchezaji huyo tena akiwa mazoezini na vijana wake kwa ajili ya kujiweka fiti.

No comments:

Post a Comment