Friday, November 18, 2011

"TEVEZ HANA NAFASI KATIKA KIKOSI CHANGU." MANCINI.

MENEJA wa Manchester City Roberto Mancini amemfungia milango mshambuliaji wake Carlos Tevez ambaye yuko kwao Argentina bila ruhusa ya klabu hiyo. Mancini alimtaka mchezaji huyo kumuomba msamaha mapema mwezi huu baada ya mchezaji huyo kukaa kupasha misuli moto katika mchezo wa Kombe la Klabu Bingwa ya Ulaya dhidi ya Bayern Munich uliochezwa mwezi Septemba mwaka huu. Meneja huyo aliondoa nafasi hiyo leo wakati akihojiwa katika mkutano na waandishi wa habari waliomuuliza kama kuna uwezekano wa mchezaji huyo kumjumuisha katika kikosi chake. Meneja huyo alijibu kuwa hakuna nafasi hiyo kwa mchezaji huyo tena.

No comments:

Post a Comment