Friday, November 18, 2011

BLATTER AOMBA RADHI.

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA Sepp Blatter ameomba msamaha kufuatia kauli yake iliyoleta mtafaruku kuhusiana na suala la ubaguzi. Bosi huyo wa FIFA Jumatano wiki hii alitoa kauli inayosema kuwa suala ubaguzi viwanjani linatakiwa kumalizwa kwa wachezaji kushikana mikono baada ya mchezo. Blatter amesema ameumizwa na bado anaumia kufuatia kauli yake hiyo iliyoleta mtafaruku na kukiri kuwa haikuwa kauli nzuri na anajutia kufanya hivyo.
Aliendelea kusema kuwa unapofanya kitu ambacho sio sahihi unachoweza kufanya ni kuomba msamaha na aliwaomba msamaha wote walioathirika kutokana na kauli kauli yake hiyo. Lakini alipoulizwa kuhusu suala la baadhi ya wadau waliomtaka ajiuzulu kutokana na kauli yake hiyo alisema haoni sababu ya kufanya hivyo.

No comments:

Post a Comment