Monday, December 19, 2011

ANZHI YASAKA KOCHA MPYA.

KLABU ya Anzhi Makhachkala ya Urusi inatarajia kuteua kocha mpya atakayeinoa klabu hiyo ifikapo mwishoni mwa mwaka huu. Akizungumza na mtandao wa klabu hiyo Mkurugenzi Mkuu aliyeteuliwa hivi karibuni Alan Soziyev amesema anawaomba mashabiki wa klabu hiyo kuwa wavumilivu kwani wako katika mchakato wa kuteua kocha mpya. Uteuzi wa Soziyev ni sehemu ya mabadiliko ya klabu hiyo ambayo inataka kupanga upya safu ya uongozi itakayoipa mafanikio klabu hiyo. Klabu hiyo hiyo inayomilikiwa na bilionea wa Urusi Suleman Kerimov imekuwa ikitajwa kuwanyemelea makocha wakubwa barani Ulaya wakiwemo Fabio Capello anayeinoa Uingereza kwasasa, meneja wa Real Madrid Jose Mourinho na kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Urusi Guus Hiddink.

No comments:

Post a Comment