Thursday, December 15, 2011

KESI YA SUAREZ KUMALIZWA KISIKILIZWA IJUMAA.

KAMATI ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka la Uingereza-FA imeanza kusikiliza mashitaka ya kibaguzi yanayomkabili mshambuliaji wa Liverpool Luis Suarez dhidi ya beki wa Manchester United Patrice Evra. Evra alifikisha mashtaka hayo akidai Suarez kumtolea kauli za kibaguzi mwezi Octoba mwaka wakati timu hizo zilipokutana na kutoa sare ya bao 1-1. Baada ya uchunguzi wa tukio hilo kufanyika FA imeamua kumshtaki Suarez kwa kutumia lugha ya kudhalilisha na kibaguzi dhidi ya beki huyo tegemeo wa Manchester United. Suarez mwenye umri wa miaka 24 amekana tuhuma hizo na amekuwa akisaidiwa na timu yake ya Liverpool muda wote wa uchunguzi huku mwisho wa kusikilizwa mashtaka hayo unatarajiwa kuwa mwishoni mwa wiki hii.

No comments:

Post a Comment