Wednesday, December 14, 2011

KOCHA WA AL SADD AOMBA KUCHEZESHA WACHEZAJI 16 DHIDI YA BARCA.

KLABU ya Al Sadd ya Qatar imelitaka Shirikisho la Soka la Dunia-FIFA kuwaruhusu kuchezesha wachezaji 16 wakati watakapokutana na mabingwa wa Ulaya Barcelona Alhamisi hii katika mchezo wa nusu fainali ya michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia. Akihojiwa kuhusiana na mchezo huo kocha wa timu hiyo raia wa Uruguay Jorge Fossati amesema mikakati yake kama watakubaliwa kuchezesha wachezaji 15 au 16 uwanjani anafikiri wanaweza kuwa na nafasi ya kuwafunga Barcelona. Nae Nahodha wa Al Sadd Abdulla Koni amesema kama Real Madrid ambao nao wanawachezaji nyota duniani wameshindwa kuwafunga Barcelona haoni kama wao wanaweza kufanya hivyo. Fainali ya ,michuano hiyo ambayo timu za Barcelona na Santos zinatabiriwa kukutana inatarajiwa kuchezwa Jumapili jijini Yokohama.

No comments:

Post a Comment