Monday, December 19, 2011

NADAL AUZA HISA ZAKE ZA MALLORCA.

MCHEZA tenisi anayeshika namba mbili dunia katika orodha ya viwango vya ubora Rafael Nadal pamoja na mjomba wake Miguel Angel Nadal wameuza asilimia 10 za hisa zao walizokuwa wakimiliki katika klabu ya Real Mallorca. Katika taarifa iliyotumwa na mtandao wa klabu hiyo hisa hizo zimenunuliwa mfanyabiashara wa Ujerumani Utz Claassen ambaye ameongoza hisa zake na kufikia asilimia 20. Nadal shabiki wa kutupwa wa klabu ya Real Madrid ambaye anaishi katika visiwa vya Mediterranean alijiunga katika kinyang’anyiro cha kununua hisa hizo mwaka 2010 wakati timu hiyo ilipokuwa katika wakati mgumu kiuchumi. Sababu kubwa ya Nadal na mjomba wake ambaye aliwahi kuwa beki wa Barcelona na timu ya taifa ya Hispania ni kutofurahishwa na uongozi wa klabu ya Mallorca unavyofanya maamuzi yake.

No comments:

Post a Comment