Sunday, December 11, 2011

SAFARI YA CHINA YANUKIA KWA ANELKA.

KLABU ya Shanghai Shenhua inayoshiriki Ligi Kuu nchini China imethibitisha Jumapili kuwa wamefikia makubaliano kuhusu mkataba wa kumsajili mshambuliaji wa Chelsea Nicolas Anelka. Msemaji wa timu ya Shanghai Ma Yue amesema kuwa wamefikiwa makubaliano juu ya mkataba wa mchezaji huyo na wanachosubiri ni yeye kutia saini na kuwa mchezaji rasmi wa klabu hiyo. Meneja wa Chelsea Andre-Villas Boas amekuwa katika katika mkakati mzito wa kukitengeneza upya kikosi cha Chelsea na tayari kuna baadhi ya nyota wa timu hiyo amewaweka sokoni ili aweze pata fedha za kukiimarisha kikosi hicho. Anelka katika kipindi cha hivi karibuni amekuwa akisumbuliwa na majeruhi kwa muda mrefu hivyo kusababisha kutokuwemo katika mipango ya kocha huyo ambaye anaonekana kuhitaji damu changa zaidi.

No comments:

Post a Comment