Sunday, December 11, 2011

GHANA KUANDAA GLO-CAF AWARDS.

SHIRIKISHO la Soka barani Afrika-CAF limethibitisha nchi ya Ghana kuandaa tuzo za Mwanasoka Bora wa Afrika kwa mwaka huu. Jiji la Accra ndio watakuwa wenyeji wa shughuli hiyo inayotarajiwa kufanyika Desemba 22 mwaka huu ambapo mbali na tuzo ya mwanasoka bora pia zitatolewa tuzo mbalimbali kwa wanamichezo waliofanya vizuri kwa mwaka huu. Hii itakuwa ni mara ya tatu kwa nchi hiyo kuandaa tafrija hiyo ambapo kwa mara ya kwanza walikuwa wenyeji wa sherehe hizo mwaka 2007 na 2009. Shirikisho la Soka nchini Ghana-GFA limefurahishwa na uteuzi huo na kdai ni heshima kubwa kwao kuandaa tafrija hiyo ambayo inatoa heshima kwa wanasoka waliofanya vizuri katika ligi mbalimbali Afrika na Duniani kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment