Sunday, January 15, 2012

CANNAVARO ATIMKIA INDIA.

NAHODHA wa zamani wa timu ya taifa la Italia iliyonyakuwa Kombe la Dunia mwaka 2006 Fabio Cannavaro ameamua kuvaa tena daruga baada ya kustaafu na kuelekea nchini India. Cannavaro ambae aliisaidia timu yake Iitalia kunyakuwa kombe hilo akiwa kama beki atakuwa sehemu ya michuano itayoshirikisha timu sita huko nchini India mashindano ambayo yameandaliwa na Chama cha Soka cha nchi hiyo wakishirikiana na kampuni ya CMG. Beki huyo atakuwa na majina mengine maarufu katika ulimwengu wa soka wakiwemo Robbie Fowler na John Barnes wa Uingereza, Mfaransa Robert Pires, Hernan Crespo na Juan Pablo Sorin wa Argentina, Fernando Morientes wa Hispania na Jay Jay Okocha wa Nigeria ni mojawapo ya sura mpya zitakazoonekana katika Ligi Kuu nchini India. Katika mtandao wa kijamii wa Twitter Cannavaro amesema kuwa ameamua kurejea uwanjani tena akiwa na klabu ya West Bengal ya nchini India lakini hakueleza ni kwa kipindi gani ataichezea klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment