Sunday, January 15, 2012

BERLUSCONI AMKUMBATIA MKWEWE PATO.

MMILIKI wa klabu ya AC Milan Silvio Berlusconi amesema ameamua kumbakisha mshambuliaji wa klabu hiyo Alexandre Pato kuliko kumuuza katika klabu ya Paris Saint-German ya Ufaransa kwa ada iliyoripotiwa kuwa kiasi cha euro milioni 35. Pato alitoa taarifa rasmi Alhamisi iliyopita kuhusu mustakabali wake wa baadae na mabingwa hao wa Serie A uamuzi huo unaonekana utasimamisha mbio za klabu hiyo za kumnyakuwa mshambuliaji wa Manchester City Carlos tevez. Katika taarifa aliyoitoa Berluscon Jumamosi amesema kuwa makubaliano ya kumuuza Pato hayakumridhisha kiufundi wala kiuchumi na anaamini maamuzi aliyochukua ni sahihi kwa klabu hiyo. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Brazil alijunga na klabu hiyo mwaka 2007 na sasa anatoka binti wa Berlusconi aitwaye Barbara.

No comments:

Post a Comment