Sunday, January 15, 2012

WENGER ADAI DIRISHA DOGO LA USAJILI LINAWAPA WACHEZAJI KIBURI.

MENEJA wa Arsenal Arsene Wenger anaamini kuwa usajili katika kipindi cha dirisha dogo unatakiwa ufutwe kwa kuwa unawapa nguvu wachezaji ambao wanakuwa hawana furaha katika timu zao. Wenger aliuambia mtandao wa klabu hiyo kuwa kwa mawazo yake dirisha dogo la usajili liondelewe na badala yake liachwe wazi kwa mwaka wote au kulifunga kwa mwaka mzima. Meneja huyo aliongeza kuwa kila mtu anakaa roho juu inapofika kipindi cha Novemba mpaka Januari halafu na wachezaji nao wanapata mawazo tofauti kwamba kama wasipocheza basi wanaweza kuondoka ikifika Januari hiyo inawapunguzia kujituma. Wenger amesema ukiwa kama mchezaji hata kama hujapangwa kucheza lakini unatakiwa kujituma kwa klabu husika katika maisha yako yote na kupigania nafasi yako katika kikosi cha kwanza.

No comments:

Post a Comment