Saturday, January 14, 2012

AVB AFURAHISHWA NA UJIO WA ESSIEN.

KIUNGO wa timu ya Chelsea jana alicheza mchezo wake wa kwanza wakati timu yake iliposhinda mchezo dhidi ya Sunderland kwa bao 1-0 katika Uwanja wa Stamford Bridge baada ya siku 273 za kuuguza majeraha. Meneja wa Chelsea Andre Villas-Boas amesema wakati akihojiwa na waandishi wa habari kabla ya mchezo huo kuwa anawapongeza madaktari waliokuwa wakimuuguza mchezaji huyo kwani kurejea kwake uwanjani mwezi mmoja kabla ni jambo la kushangaza. Kiungo huyo wa Kimataifa wa Ghana aliingia katika dakika ya 73 akichukua nafasi ya Frank Lampard na kwa muda mfupi alioingia alibadilisha mchezo juhudi ambazo zilizaa matunda dakika chache baadae. Essien mwenye umri wa miaka 29 aliumia mwanzoni mwa msimu wa ligi majeraha ambayo yamemuweka nje ya dimba kwa muda miezi sita na hatakuwa sehemu ya kikosi cha Ghana kitakachoshiriki michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya makubaliano kwamba lazima apone kabisa ili atumike katika majukumu ya kimataifa.

No comments:

Post a Comment