Friday, January 13, 2012

RIVALDO KUTIMKIA ANGOLA.

MCHEZAJI nyota wa zamani wa Brazil Rivaldo amethibitisha kuwa yuko njiani kujiunga na klabu ya Kabuscorp inayoshiriki Ligi Kuu nchini Angola. Rivaldo mwenye umri wa miaka 39 aliachwa na klabu ya nchini kwao ya Sao Paulo baada ya kuitumikia kwa muda wa miezi 12 tu lakini mwenyewe bado anapenda kucheza soka mpaka mwishoni mwa mwaka huu. Mchezaji huyo anayecheza nafasi ya kiungo tayari ameshashinda mataji mengi katika kipindi chake cha uchezaji soka ikiwemo Kombe la Dunia mwaka 2002, Klabu Bingwa ya Ulaya akiwa na AC Milan mwaka 2003 na tuzo ya mchezaji bora wa Dunia na Ulaya mwaka 1999. Akithibisha habari hizo Rivaldo amesema ni kweli yuko katika mazungumzo na klabu hiyo na anatarajia kusafiri kuelekea huko kuangalia kama wanaweza kufikia makubaliano.

No comments:

Post a Comment