Friday, January 13, 2012

GAUCHO ATISHIA KUIKACHA FLAMENGO.

Mshambuliaji wa kimataifa wa Brazil Ronaldinho Gaucho ametishia kuikacha klabu yake ya Flamengo kama hawatamlipa mshahara wake unaofikia kiasi cha dola milioni mbili. Katika taarifa iliyotolewa na wakala wake ambaye pia ni kaka yake Roberto de Assis imesema kuwa wanataka kufikia makubaliano kuhusu suala hilo ili Ronaldinho aweze kushiriki michuano ya Klabu Bingwa ya Amerika Kusini maarufu kama Copa Libertadores. Robo tatu ya mshahara wa mchezaji huyo inalipwa na Kampuni ya Masoko ya Traffic ambao hawajalipa kwa muda wa miezi mitano sasa kiasi kinachofikia dola milioni mbili na zaidi. De Assis alionya kuwa kama mchezaji huyo ambaye ana umri wa miaka 31 hatalipwa fedha hizo haraka atakubali moja ya maombi kutoka katika timu za aidha Italia, Hispania au Amerika Kusini zinazomuwania mshambuliaji huyo.

No comments:

Post a Comment