Monday, January 16, 2012

MARADONA ALAZWA DUBAI.

KLABU ya Al Wasl ya Dubai imetangaza kuwa kocha wake mkuu Diego Maradona amelazwa katika Hospitali moja nchini humo baada ya kugundilika kuwa na mawe katika figo yake. Maradona mwenye umri wa miaka 51 alienda hospitalini hapo mapema Jumapili iliyopita kwa ajili uchunguzi na kwasasa amewekwa katika uangalizi ili baadae aweze`kufanyiwa upasuaji kuondoa mawe hayo. Msemaji wa klabu ya Al Wasl amesema kuwa mchezaji huyo alikuwa akijisikia maumivu kabla ya kupelekwa hospitalini hapo ambapo alitarajiwa kufanyiwa upasuaji Jumapili jioni kabla ya kuruhusiwa leo. Klabu hiyo ilitarajiwa kutoa taarifa zaidi kuhusu afya ya Maradona inavyoendelea baadae leo.

No comments:

Post a Comment