Wednesday, February 15, 2012

AMRI ZAKI AIHOFIA YANGA.

MSHAMBULIAJI wa Zamalek Amr Zaki ametoa tahadhari kufuatia mchezo wao Klabu Bingwa ya Afrika dhidi ya Yanga akidai kuwa utakuwa mchezo mgumu mchezo ambao utachezwa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Zaki amesema kuwa mchezo huo utakuwa mgumu hivyo inabidi wawe tayari kwa hilo na kama wakifanikiwa kushinda mchezo huo basi mchezo unaofuatia utakuwa rahisi kidogo kwao. Mshambuliaji huyo aliendelea kusema kuwa lazima waiheshimu Yanga kwasababu watakuwa wakicheza nyumbani mbele ya mashabiki wao hivyo kuwafanya wawe hatari kwa mchezo huo. Zaki ambaye ana umri wa miaka 28 ameshinda mabao mawili katika michezo miwili ya kirafiki Zamaleki iliyocheza dhidi ya timu ya Telcom ya nchini humo ambapo wanatarajiwa kusafiri kuja Tanzania kesho kwa ajili ya mchezo huo wa Jumamosi.

No comments:

Post a Comment