Monday, February 27, 2012

DALGLISH ATAMBA KULETA VIKOMBE ZAIDI ANFIELD.

MENEJA wa Liverpool Kenny Dalglish anaamini kuwa kikosi chake kitajijenga baada ya ushindi wa Kombe la Ligi dhidi ya Cardiff jana na kuleta vikombe vingi zaidi hapo Anfield. Liverpool walifanikiwa kuwashinda wapinzani wao kwa changamoto ya mikwaju ya penati mwishoni mwa mchezo huo na Dalglish anafikiria ushindi huo utaoneza hamasa kwa wachezaji ili kutafuta vikombe zaidi. Akihojiwa kocha huyo mwenye umri wa miaka 60 ushindi huo ambao umemaliza ukame wa miaka sita ambayo klabu hiyo utakuwa ni chachu ya kupata mafanikio zaidi na vikombe vingi zaidi katika siku za mbeleni. Dalglish ambaye ni raia wa Scotland ni mmoja kati ya makocha saba wanaofundisha vilabu vya Ligi Kuu Uingereza ambaye ameshashinda mataji matatu makubwa ya Ligi Kuu nchini humo.

No comments:

Post a Comment