Monday, February 20, 2012

GUARDIOLA MGUU NJE MGUU NDANI BARCA.

MENEJA wa klabu ya Barcelona Pep Guardiola amesema kuwa bado hajaamua kama ataendelea kuinoa kikosi cha timu hiyo baada ya msimu huu kumalizika. Akiwa na kikosi hicho Guardiola mwenye umri wa miaka 41 ameshinda mataji 13 katika ya 16 toka alichukua kibarua cha kuinoa klabu hiyo miaka minne iliyopita na kusema kuwa bado hajaamua kama atalendelea kuinoa klabu hiyo au atondoka. Meneja huyo amesaini mkataba wa mwaka mmoja na klabu hiyo baada ya kukubali kuendelea kukaa klabuni hapo kwa miaka mingine miwili zaidi lakini akasema uongozi wa klabu hiyo haujampa masharti yoyote. Nafasi ya Guardiola imekuwa haieleweki kwa mabingwa hao wa Hispania kwasababu kocha huyo amekuwa akiongeza mkataba katikati ya msimu kwa miaka miwili iliyopita.

No comments:

Post a Comment