Sunday, February 12, 2012

SENEGAL YAMWINDA HERVE RENARD.

SHIRIKISHO la Soka nchini Senegal-FSF limesema liko katika mipango ya kujaribu kuzungumza na kocha wa Zambia Herve Renard mwenye miaka 43 ili aibe pengo la Amara Traore ambaye alifukuzwa wiki iliyopita baada ya timu hiyo kutolewa mapema katika michuano ya Kombe la Matifa ya Afrika. Rais wa FSF Augustin Senghor aliwasili Gabon Alhamisi iliyopita kwa ajili ya mkutano mkuu wa Shrikisho la Soka barani Afrika-CAF ambapo alitarajia kuanzisha mawasiliano na kocha huyo. Maofisa wa Senegal wanahitaji kocha ambaye ana uzoefu na soka la Afrika ili kuendelea pale alipoishia Traore. Renard ambaye alishawahi kuinoa klabu ya USM Alger ya Algeria ndio anayepewa nafasi kubwa ya kuchukua mikoba ya Traore lakini haijafahamika kama kocha huyo ataacha kukinoa kikosi cha Zambia baada ya michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment