Friday, March 16, 2012

CHAMPIONS LEAGUE DRAW.

TIMU ya AC Milan ya Italia imepangwa kukutana na Barcelona ya Hispania katika robo fainali ya michuano ya Kombe la Klabu Bingwa ya Ulaya. Katika droo hiyo iliyopangwa leo na Shrikisho la Soka Barani Ulaya Real Madrid itakutana kwa mara ya kwanza na timu ngeni katika hatua ya Apoel Nicosia ya Ugiriki huku Olympic Marseille ya Ufaransa nayo kwa mara kwanza itaikaribisha Bayern Munich katika mchezo wa kwanza wa michuano hiyo. Timu pekee ya Uingereza katika hatua hiyo msimu huu Chelsea wao wataanzia ugenini katika mchezo wa kwanza wakicheza na Benfica ya Ureno. Mshindi kati ya Chelsea na Benfica atakutana na mshindi kati AC Milan au Barcelona katika hatua ya nusu fainali huku mshindi kati ya Real Madrid na APOEL atakutana na mshindi kati ya Marseille na Bayern Munich kwenye hatua kama hiyo.

No comments:

Post a Comment