Wednesday, March 21, 2012

FAINALI UEFA CHAMPIONS LEAGUE 2013/14 KUPIGWA ESTADIO DA LUZ, LISBON, URENO.

Estadio da Luz
KAMATI ya Utendaji ya Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA limeuteua Estadio da Luz au Uwanja wa Taa uliopo katika jiji la Lisbon, Ureno kutumika mchezo wa fainali ya Kombe la Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu wa 2013-2014. Kwa mara ya mwisho jiji hilo kuandaa fainali hiyo ilikuwa ni mwaka 1967 enzi hizo kombe hilo likiitwa Kombe la Ulaya mwaka 1967 ambapo Celtic iliichabanga Inter Milan mabao 2-1 katika mchezo wa fainali ya michuano hiyo. Fainali za Ligi ya Ulaya au Europa League msimu wa mwaka 2013-2014 itafanyika katika jiji la Turin nyumbani kwa timu ya Juventus ya Italia ambapo fainali hiyo itwapigwa katika uwanja mpya wa klabu hiyo ambao umefunguliwa mapema msimu huu. Wakati michuano ya Kombe la Mataifa ya Ulaya mwaka 2015 kwa vijana chini ya umri wa miaka 21 itafanyika Jamhuri ya Czech.

No comments:

Post a Comment