Wednesday, March 21, 2012

COYLE AZUNGUMZA NA MUAMBA.

MENEJA wa klabu ya Bolton Wanderers Owen Coyle amesema amezungumza kwa ufupi na mchezaji Fabrice Muamba mwa mara ya kwanza toka alipopoteza fahamu Jumamosi iliyopita kutokana na matatizo ya moyo. Mchezaji huyo amelazwa katika Hospitali ya London Chest baada ya kuanguka na kupoteza fahamu katika mchezo baina ya timu hiyo na Tottenham Hotspurs wa robo fainali ya Kombe la Chama cha Soka nchini Uingereza-FA. Coyle amesema kuwa mchezaji huyo bado ana safari ndefu ya kupona kabisa lakini maendeleo yake yanatia moyo ukilinganisha na hali aliyokuwa nayo Jumamosi wakati tukio hilo lilipotokea. Madaktari wanaomhudumia Muamba ambaye ameshawahi kucheza katika kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza cha vijana chini ya umri wa miaka 21 wamesema kuwa hali yake inaendelea vizuri ingawa bado wataendelea kumuangalia kwa karibu ili kujua maendeleo yake.

No comments:

Post a Comment