Sunday, March 18, 2012

KLINSMANN AICHOMOLEA TOTTENHAM.

KOCHA Mkuu wa timu ya taifa ya Marekani Jurgen Klinsmann amesema hawezi kuachia nafasi yake hiyo kwenda Uingereza kuifundisha klabu ya Tottenham Hotspurs. Meneja wa sasa wa Tottenham Harry Redknapp ndio anapewa nafasi kubwa ya kuwa kocha mpya wa timu ya taifa ya Uingereza baada ya aliyekuwa kocha wa klabu hiyo Fabio Capello kujiuzulu Februari mwaka huu. Pamoja na klabu hiyo kumuweka kocha huyo katika orodha ya watu ambao watamrithi Redknapp kama akiondoka, Klinsmann ambaye amewahi kuitumikia klabu hiyo katikati ya miaka ya 90 amesisitiza kuwa hana mpango wa kuondoka Marekani kwasasa. Klinsmann alipewa mikoba ya kuinoa timu ya Marekani katika mkataba wa miaka mitatu akichukua nafasi ya Bob Bradley Julai mwaka jana.

No comments:

Post a Comment