Saturday, March 24, 2012

VURUGU ZAISABABISHIA ADHABU GOR MAHIA.

BODI ya Viwanja vya Michezo nchini Kenya (SSMB) imeifungia klabu ya Gor Mahia kutumia Viwanja vya Nyayo na Moi International Sports Centre Kasarani. Hatua hiyo inakuja baada ya vurugu za mwishoni mwa wiki katika mechi yao na wapinzani wao wa jadi, AFC Leopards ambayo ilivunjika baada ya dakika 26 tu. Uamuzi huo umefikiwa kutangazwa na Mwenyekiti wa bodi hiyo, Generali Mstaafu Daniel Opande. Pamoja na hayo, uamuzi hao haupokewa vizuri na Gor Mahia ambayo imechukuliwa kama ni wa haraka. Kifungo hicho kinawafanya Gor Mahia wawe na Uwanja mmoja tu wa kutumia, City ambao hauendani na idadi kubwa ya mashabiki wao

No comments:

Post a Comment