Monday, April 23, 2012

ADRIANO KUISHITAKI CORINTHIANS.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa Corinthians, Adriano ameelezea nia yake ya kuchukua hatua za kisheria kwa klabu yake hiyo akidai kuwa walimfanya mfungwa wakati klabu hiyo ilipomfungia hotelini na kumpa mazoezi ya kupunguza uzito kwa muda wa wiki moja. Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 30 amesema hayo wakati akihojiwa na luninga moja nchini Brazil akimtupia lawama kocha wa klabu hiyo akisema kuwa wamemwacha huku wakiwa wamemdhalilisha. Aliendelea kusema kuwa atachukua hatua za kisheria kwa klabu hiyo kwa kumuweka kama mfungwa kwa wiki moja kitendo ambacho hakuwa ameridhika nacho hivyo aliona kama adhabu. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Inter Milan katika mahojiano hayo amekiri kuwa na matatizo kutokana na kuongezeka uzito wakati akiichezea klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment