Monday, April 23, 2012

UKRAINE HATARINI KUMKOSA NA GOLIKIPA WAKE WA TATU.

TIMU ya taifa wa Ukraine ambao ni wenyeji wenza wa michuano ya Ulaya 2012 iko katika hatari ya kumpoteza golikipa wake wa tatu baada ya Oleksandr Shovkovskiy anayecheza katika klabu ya Dynamo Kiev kuumia bega wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya nchi hiyo jana. Kocha Mkuu wa Kiev, Yuri Syomin amesema kuwa mchezaji huyo atafanyiwa vipimo zaidi ilikujua ukubwa wa tatizo lake lakini kwa jinsi inavyoonekana tatizo linaweza kuwa kubwa. Kuumia kwa kipa huyo itakuwa ni pigo kwa kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo kutokana na kuwapoteza makipa wengine wazoefu wawili. Oleksandr Rybka ambaye ndiye kipa chaguo la kwanza katika kikosi hicho amefungiwa kutokana na kutumia madawa ambayo yamekatazwa michezoni wakati Andriy Dykan ambaye ndiye chaguo la pili yeye amevunjika mkono wakati mechi mwezi uliopita. Katika michuano ya Ulaya ambayo Ukraine imeandaa kwa pamoja na Poland imepangwa kundi na timu za Uingereza, Ufaransa na Sweden katika kundi D.

No comments:

Post a Comment