Monday, April 23, 2012

VAN PERSIE WIN PFA PLAYER AWARD.

MSHAMBULIAJI wa Arsenal, Robin van Persie ametajwa kuwa mchezaji bora wa mwaka wa kulipwa katika Ligi Kuu nchini Uingereza. Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 28 amefunga mabao 38 msimu huu yakiwemo mabao 34 katika mashindano yote akiwa na klabu ya Arsenal. Akihojiwa mara baada ya kupokea tuzo hiyo mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi ambaye kwasasa ndiye anayeongoza kwa ufungaji katika ligi hiyo amesema tuzo hiyo ni kitu muhimu sana kwake na aliwashukuru wachezaji wenzake kwani bila ushirikiano wao asingefika hapo alipo. Van Persie amenyakuwa tuzo hiyo mbele ya mshambuliaji wa Manchester United Wayne Rooney, Scott Parker wa Tottenham Hotspurs na Sergio Aguero, Joe Hart na David Silva wote wa Manchester City.

No comments:

Post a Comment