Sunday, April 22, 2012

KUPONA KWANGU NI ZAIDI YA MAAJABU-MUAMBA.

KIUNGO wa klabu ya Bolton Wanderers, Fabrice Muamba amesema kuwa kupona kwake kufuatia ugonjwa wa moyo wake kusimama ghafla ni zaidi ya maajabu ambayo hayakutegemewa. Muamba mwenye umri wa miaka 24 aliongea na gazeti la Sun la Uingereza kwa mara ya kwanza toka mapigo yake ya moyo yaliposimama kwa dakika 178 baada ya kuanguka wakati wa mchezo dhidi ya Tottenham Hotspurs mwezi uliopita. Mchezaji huyo amesema kuwa kilichomtokea ni maajabu kwani asubuhi kabla ya mchezo huo alienda kwenye maombi na baba yake na kumuomba mungu amlinde na alifanya hivyo baada kumponya na umauti baada ya kuanguka jioni yake. Muamba aliruhusiwa kutoka hospitalini Jumatatu iliyopita baada ya kuonyesha kupona vizuri ikiwa ni zaidi ya mwezi toka alipoanguka ingawa haijajulikana kama mchezaji huyo atarejea tena kucheza soka katika siku za mbeleni.


No comments:

Post a Comment