Sunday, April 22, 2012

BLATTER AMTEMBELEA MWENZAKE.

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Sepp Blatter amemtembelea rais aliyemtangulia Joao Havelange ambaye amelazwa kwa zaidi ya mwezi katika hospitali moja jijini Rio de Janeiro, Brazil. Blatter aliandika taarifa ya kwenda kumtembelea Havelange katika mtandao wake wa kijamii wa Twitter kuwa alikuwa katika safari binafsi yeye pamoja na binti yake aitwaye Carinne wakielekea hospitalini Rio De Janeiro kumtembelea Havelange. Madaktari katika hospitali ya Samaritano anapotibiwa Havelange wamesema kuwa kifundo cha mguu wa kulia ambacho ndicho kilichosababisha kulazwa kwa rais huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 95 tayari umepona kwasasa bado anatumia dawa kujaribu kutibu matatizo ya moyo ambayo yalimkumba karibuni. Mara baada ya kumuona Havelange ambaye aliwahi kuingoza FIFA kuanzia mwaka 1978 mpaka 1998, Blatter aliandika katika mtandao huo kuwa amefurahi kuona anaendelea vizuri na ana matumaini atapona kabisa na kuendelea na shughuli zake.

No comments:

Post a Comment