Sunday, April 22, 2012

MADRID WAVUNJA REKODI YAO WENYEWE.

KLABU ya Real Madrid imefanikiwa kuvunja rekodi ya mabao katika Ligi Kuu ya Hispania kwa msimu mmoja baada ya kufanikiwa kuwafunga mahasimu wao Barcelona kwa mabao 2-1. Bao la Sami Khedira alilofunga katika dakika ya 17 liliifanya timu hiyo kufikisha mabao 108 katika msimu huu wakivunja rekodi yao wenyewe ya mabao 107 waliyoiweka katika msimu wa mwaka 1989-1990 wakati kikosi hicho kikinolewa na Hugo Sanchez kutoka Mexico. Mshambuliaji wa Madrid Cristiano Ronaldo alifanikiwa kuongeza bao lingine la ushindi dakika ya 73 na kufanikiwa kufikisha mabao 42 katika msimu huu ikiwa ni bao moja zaidi ya mpinzani wake Lionel Messi ambaye ana mabao 41. Katika msimu wa 1989-1990 Madrid walifanikiwa kushinda taji la ligi kuu ikiwa ni taji lao la tano mfululizo kushinda katika kipindi hicho.

No comments:

Post a Comment