Sunday, April 22, 2012

WELBECK ASAINI MKATABA MREFU NA UNITED.

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Manchester United Danny Welbeck anatarajiwa kutia saini ya mkataba wa miaka mitano mwishoni mwa msimu huu baada ya kufikia makubaliano na klabu hiyo. Welbeck mwenye umri wa miaka 21 amekubali kusaini mkataba huo utakaomuwezesha kuwa akilipwa kiasi cha paundi 45,000 kwa wiki. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza ambaye mkataba wake wa awali unaisha mwishoni mwa msimu huu aliwaambia wachezaji wenzake kuwa amefurahishwa na kusaini mkataba mrefu na klabu hiyo kabla hajakwenda kuitumikia nchi yake katika michuano ya Ulaya baadae mwaka huu. Welbeck ambaye msimu uliopita alipelekwa kwa mkopo katika klabu ya Sunderland, amefunga mabao 11 katika mashindano yote msimu huu huku akichukua nafasi ya Dimitar Berbatov na Juvier Hernandez kama chaguo la kwanza kwa washambuliaji wa klabu hiyo ambaye anaweza kucheza sambamba na Wayne Rooney.

No comments:

Post a Comment