Tuesday, April 24, 2012

BRITAIN, SPAIN, BRAZIL, MEXICO SEEDED.

TIMU za Uingereza ambao ndio wenyeji wa michuano ya Olimpiki, Hispania ambao ni mabingwa wa dunia, Brazil na Mexico zimetajwa na Shirikisho la Soka la Dunia-FIFA kuongoza makundi yao kati ya timu 16 za soka za wanaume zitakazoshiriki michuano hiyo katika ratiba itakayopangwa baadae leo. Kwa upande wa wanawake ambapo kutakuwa na timu 16, Uingereza, Japan ambao ni mabingwa wa dunia kwenye soka la wanawake, na bingwa mtetezi wa michuano hiyo Marekani wao ndio watakaoongoza makundi yao katika soka la wanawake katika michuano hiyo. Katika michuano hiyo kwa upande wa wanaume timu 16 zitagawanywa katika makundi manne ambapo Uingereza itaongoza kundi A kwa mara ya kwanza toka walipoandaa michuano hiyo mwaka 1960. Mexico wenyewe wataongoza kundi B wakati Brazil ambao nndio timu pekee ambayo ina rekodi nzuri na michuano hiyo pamoja na kwamba hawajawahi kupata medali ya dhahabu wataongoza kundi C na Hispania wataongoza kundi D.

No comments:

Post a Comment