Tuesday, April 24, 2012

SENEGAL YAFUZU OLIMPIKI.

TIMU ya taifa wa Senegal ya vijana chini ya miaka 23, imekuwa timu ya mwisho kukata tiketi ya kucheza michuano ya Olimpiki baada ya kufanikiwa kuifunga Oman kwa mabao 2-0 katika mchezo uliochezwa jijini Coventry, Uingereza. Bao kuongoza la Senegal lilifungwa katika dakika za mwanzo za mchezo kupitia mpira wa adhabu wa adhabu uliopigwa na Pape Ndiaye Souare anayecheza katika klabu ya Lille ya nchini Ufaransa kabla ya Ibrahima Balde kumalizia anayecheza klabu ya Osasuna ya Hispania kumalizia mpira huo kwa kichwa. Mara baada ya bao hilo Oman walionekana kuongeza mashambulizi ili kurejesha bao hilo juhudi ambazo hazikuzaa matunda baada ya kiungo Abdoulaye Sane anayecheza katika klabu ya Rennes nayo ya Ufaransa kuipatia timu yake bao la pili katika dakika 86 na kuzima ndoto za za Oman kushiriki michuano hiyo. Senegal inashiriki michuano hiyo kwa mara ya kwanza wakati watakapojumuika na timu zingine 14 ambazo tayari zimefuzu michuano hiyo ambazo ni Korea Kusini, Japan, Umoja wa Falme za Kiarabu-UAE, Gabon, Morocco, Misri, Uingereza, Hispania, Switzerland, Belarus, Honduras, Mexico, New Zealand, Brazil na Uruguay.

No comments:

Post a Comment