Tuesday, April 24, 2012

SENEGAL FOOTBALL FEDERETION ACCOUNTS FROZEN.

SHIRIKISHO la Soka la Senegal-FSF limefungiwa akaunti zake kwa maagizo ya mahakama ya jijini Dakar kufuatia kesi waliyofunguliwa na kocha wa zamani wa timu ya taifa ya nchi hiyo Amara Traore. Rais wa FSF Augustin Senghor aliwapa taarifa hizo waandishi wa habari nchini humo kwa njia ya simu kutoka jijini Coventry, Uingereza ambapo timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 23 ya nchi hiyo ilifanikiwa kuifunga Oman na kufanikiwa kufuzu michuano ya Olimpiki itakayofanyika jijini London mwaka huu. Mahakama ya Saint Louis iliyopo Kaskazini mwa Senegal mapema mwezi huu iliamuru FSF kumlipa Traore Francs milioni 36 zikiwa ni pesa za malimbikizo ya mshahara wa miezi miwili pamoja na posho za likizo. Traore alitimuliwa kukinoa kikosi cha nchi hiyo baada ya kutolewa katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika Januari mwaka huu ambapo walitolewa katika hatua ya makundi.

No comments:

Post a Comment