Friday, April 20, 2012

CHELSEA KATIKA KIBARUA KINGINE EMIRATES STADIUM.

BAADA ya ushindi walioupata dhidi ya Barcelona Jumatano, Chelsea wanatarajiwa kuwa na kibarua kingine kesho wakati wataposafiri kuifuata Arsenal katika mchezo wa Ligi Kuu nchini Uingereza utakaofanyika katika Uwanja wa Emirates. Arsenal ambao wanakamata nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi hiyo wameizidi Chelsea ambao wanashika nafasi ya sita kwa alama saba lakini wakiwa na mchezo mmoja zaidi, lakini kufungwa kwa timu hiyo na Wigan Athletic Jumatatu kumetoa nafasi kwa timu nne kuwa katika nafasi ya kugombania nafasi ya tatu na nne kwa ajili ya michuano ya Ligi ya Mabingwa. Arsenal itaingia uwanjani bila ya kiungo wake Mikel Arteta ambaye ana majeraha katika kifundo chake cha mguu aliyopata wakati wa mchezo dhidi ya wigan. Tottenham Hotspurs ambao wanashika nafasi ya nne baada ya kusuasua katika michezo yao ya hivi karibuni wao watasafiri kuifuata Queens Park Rangers. Mbio za ubingwa zitakuwa Jumapili ambapo Manchester United itakapopata nafasi ya kusogeza pengo la pointi wakati wakakapocheza na Everton majira ya mchana wakati mahasimu wao Manchester City wao watacheza na Woverhampton Wanderers jioni.

No comments:

Post a Comment